Ijumaa, 24 Aprili 2015
MWILI WA MWANAFUNZI KITETO ALIYEFARIKI KWA KUCHAPWA VIBOKO NA WALIMU WAFIKISHWA DODOMA
MWILI wa mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari Matui
iliyoko Wilaya ya Kiteto, Mkoa wa Manyara, aliyedaiwa kufariki baada ya
kuchapwa viboko na walimu wake, Emmanuel Mbigima (15), umefikishwa
katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma.
Wakati mwili huo unafikishwa hospitalini hapo jana asubuhi, ulikuwa
umewekwa kwenye gari la Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto ukisindikizwa na
baadhi ya ndugu wa karibu wa familia ya marehemu.
Akizungumza na waandishi wa habari hospitalini hapo, babu wa marehemu,
Emmanuel Ngowi, alisema mwili huo umeletwa hospitalini hapo kwa ajili ya
kufanyiwa vipimo ambavyo vimekosekana katika hospitali ya Wilaya ya
Kiteto.
"Mjukuu wangu alipigwa na walimu watatu tarehe 20 mwezi huu kutokana na kufeli mtihani wa somo la Kiswahili.
“Tumechukua uamuzi wa kumleta hapa kwa sababu madaktari wa Hospitali ya
Wilaya ya Kiteto, walishindwa kubaini kichwa kimeathirika kwa kiasi gani
kwa kuwa hawana vifaa vya uchunguzi vya kichwa.
“Hata hivyo, majibu ya uchunguzi wa awali yaliyotolewa katika hospitali
hiyo, yalionyesha jicho la kulia lilivuja damu kwa ndani na pia mwili wa
marehemu ulikuwa na michubuko miguuni,” alisema Ngowi.
Naye mjomba wa marehemu, Michael Ezekiel alisema matukio ya wanafunzi
kupigwa na kupoteza maisha yamekuwa yakijirudia shuleni hapo kwa kuwa
hakuna hatua zinazochukuliwa dhidi ya watuhumiwa.
“Mwaka jana kuna mtoto alipigwa na mwalimu akafariki, lakini mtuhumiwa
alipelekwa mahakamani na baadaye kuachiwa kwa madai kuwa mtoto alikuwa
ni mgonjwa,” alisema.
Kwa upande wake, Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Dodoma,
Dk. Zainabu Chaula, alithibitisha kupokelewa kwa mwili huo na kusema
uchunguzi bado unaendelea.
Awali, akizungumza na MPEKUZI baada ya mwanafunzi huyo kufariki, Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Manyara, Christopher Fuime, aliwataja walimu
waliohusika katika tukio hilo na ambao wanashikiliwa na Jeshi la Polisi,
kuwa ni Machael Bajutta (28), Chalamilla Gereza (33) na Mwalimu Joyce
Msiba (36).
Je,huyu ndio mwanamke mrembo duniani?
Huenda asijihisi kuwa mrembo ,lakini Sandra Bullock ndiye mwanamke mrembo duniani.
Iwapo anaamini hilo au la ,nyota huyo wa filamu mwenye umri wa miaka 50 ametangazwa na gazeti la People magazine kama chaguo lake la kila mwaka la mwanamke mrembo duniani mwaka 2015.Msanii huyo alidokezewa kuhusu habari hiyo kabla ya tangazo hilo kutolewa na jarida hilo.
Je tunakuuliza unakubaliana na uamuzi wa gazeti hilo kwamba Sandra Bullock ndiye mwanamke mrembo duniani?
VIDEO YA ‘NUSU NUSU’ YA JOH MAKINI IMEANZIA KWENYE TV KUBWA DUNIANI YA MTV.. STORI IKO HAPA
Kingine ambacho nimekishuhudia muda mfupi uliopita kwenye Channel
ya MTV #322 on DSTV ni hii video ya Mbongo mwingine.. Mkali wa Hiphop
toka kundi la WEUSI, Joh Makini ikitambulishwa rasmi kwa mara ya kwanza.
Wimbo unaitwa Nusu Nusu, Joh kamshirikisha mweusi mwingine mkali wa
Chorus, G Nako.
Ni furaha kumuona mwana Hiphop kwenye Headlines za TV kubwa...
Hii ndio Taarifa ya Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro kuhusu Tukio la Majambazi kuua na Kupora Fedha April 20,2015.
UHALIFU:-

Majambazi
yaliyokuwa na silaha yalivamia gari mali ya Kampuni ya Bonite na kuwamiminia
risasi dereva wa gari hilo na mlinzi wa
Kampuni hiyo kisha kupora fedha na kutokomea
kusikojulikana.
Taarifa
zinadai kuwa dereva na mlinzi wa gari lililoshambuliwa walifariki palepale
kutokana na kupigwa risasi nyingi sehemu mbalimbali za miili yao.
Tukio hilo
limetokea April 20, 2015 mjini Moshi ambapo majambazi wanne waliokuwa kwenye
pikipiki walivamia gari la Bonite lililokuwa likitoka kuchukua pesa za mauzo ya
kampuni hiyo.

Tukio hilo
limetokea April 20, 2015 mjini Moshi ambapo majambazi wanne waliokuwa kwenye
pikipiki walivamia gari la Bonite lililokuwa likitoka kuchukua pesa za mauzo ya
kampuni hiyo.

Alhamisi, 23 Aprili 2015
VPL 2014/2015:-Ijumaa April 23, 2015 Yanga SC v Ruvu Shooting huku mechi mbili tu Kuwapa Ubingwa wa Msimu huu.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)
https://www.youtube.com/watch?feature=player_embedded&v=zrlC-BViZxw.
