Wanafunzi wa Kozi ya Mafunzo ya Upigaji wa Picha na Photoshop Wamuaga Mkufunzi wao kutoka JICA Japan
Ofisa Muandamizi wa
Idara ya Habari Maelezo Zanzibar Ndg.
Faki Mjaka akizungumza wakati wa hafla
hiyo ya kumuaga Mtaalam wa Mafunzo ya Upigaji Picha kutoka Japan Mr Hiro,
iliyotayarishwa na Wanafunzi hao na kumzawadia zawadi mbalimbali wakati wa hafla
hiyo.
Mr. Hiro Mtaalam wa mafunmzo ya Upigaji wa Picha za Mnato
kutoka Shirika la Kujitolea la Japani (JICA) akiwa makini akimsikiliza Ofisa wa Maelezo Zanzibar
akitowa shukrani kwa mkufunzi hiyo, wakati wa hafla iliyofanyika katika ukumbi
wa hoteli ya Kipangani Café Nungwi Zanzibar.
Mr.Hiro Matsuda akizungumza na Wanafunzi wake wakati wa hafla ya kumuaga
iliyofanyika katika Hoteli ya Kipangani Cafe Nungwi Zanzibar, akitowa
shukrani kwa wanafunzi hao wakati wote wa mafunzo yake yaliyochukua miaka
miwili ya masomo
Wanafunzi wa Kozi ya Upigaji Picha wakimsikiliza Mr Hiro
akitowa nasaha zake kwa Wanafunzi wake
baada ya kumuandalia hafla maalum ya
kumuaga iliyofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Kipangani Café Nungwi Zanzibar.
Mkufunzi
Mkuu wa Mafunzo ya Upigaji Picha kwa Wafanyakazi wa Idara mbalimbali za
Serikali na Binafsi wakimsikiliza Mr Hiro Matsuda.
Mmoja wa Wanafunzi wa Kozi ya Upigaji wa Picha kutoka Idara
ya Habari Maelezo Zanzibar Bi Fatma, akimkabidhi kasha ikiwa ni zawadi kutoka kwa Wanafunzi wa
Darasa hilo, Mr Hiroi Matsuda amemaliza muda wake Zanzibar baada ya kutoa
mafunzo kwa muda wa miaka miwili. Mwanafunzi wa Darasa la Mr Hiro Matsuda Ndg Shibli Haji
Shibli akimkabidhi zawadi ya fulana yenye ujumbe Hakuna
Matata Zanzibar, zawadi hizo zimetolewa na Wanafunzi wa Kozi hiyo.
Mwanafunzi wa Darasa la Mr Hiro Matsuda Bi Miza Omar akimkabidhi
zawadi ya Mlango wa Zanzibar zawadi hizo zimetolewa na Wanafunzi wa Kozi hiyo.
Ofisa Muandamizi wa Idara ya Habari Maelezo Zanzibar na
Msemaji wa Timu ya Shaba Wazee wa Dago Ndg Faki Mjaka akimkabidhi Mr Hiro
Matsuda, ikiwa ni kumbukumbu yake kutoka katika Uongozi wa timu hiyo, Mr. Hiro
amebuni Nembo ya Timu hiyo ikiwa katika fulana hiyo na inatumiwa na timu hiyo
rasmin kwa sasa.
Wanafunzi wa darasa la Mr Hiro la Upigaji Picha wakiwa katika ufukwe wa nungwi kwa ajili ya
kumuaga mwalimu wao baada ya kumaliza mafunzo ya Upigaji wa Picha na Photoshop,
yaliYochukua miaka miwili .
Wanafunzi wa Kozi ya Upigaji picha na Photoshop wakifurahia wakiwa katika ufukwe wa Nungwi.
Mr. Hiro katika pozi maeneo ya jabali la hoteli ya
Nungwi akiwa na Mwanafunzi wake Othman. Wakiwa katika picha ya kumbukumbu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni